a 1Sam 12:25; Kum 4:27; 2Fal 24:14; 2Fal 25:7-11; 2Nya 33:11; 2Nya 36:21; Ezr 5:12; Yer 15:14; 16:13; 27:20; 29:1-9; 52:28; Mao 1:3; Kum 4:28
b Yer 42:18; Eze 5:15; Za 22:7; 39:8; 44:13; 64:8; Yer 18:16; 48:27; Mik 6:16; 2Nya 7:20; Ezr 9:7; Yer 44:8; 1Fal 9:7; Za 44:14; Yer 19:8; 24:9; 25:9, 18; Yer 29:18; Mao 2:15
Deuteronomy 28:36-41
36 a Bwana atakupeleka wewe na mfalme uliyemweka juu yako uende kwenye taifa ambalo hukulijua wewe wala baba zako. Huko utaabudu miungu mingine, miungu ya miti na mawe. 37 bUtakuwa kitu cha kuchukiza, tena kitu cha kudharauliwa na kudhihakiwa kwa mataifa yote huko Bwana atakakokupeleka. 38 cUtapanda mbegu nyingi katika shamba lakini utavuna haba, kwa sababu nzige watazila. 39 dUtapanda mashamba ya mizabibu na kuyapalilia, lakini hutakunywa divai yake wala hutakusanya zabibu, kwa sababu wadudu watazila. 40 eUtakuwa na mizeituni katika nchi yako yote, lakini hutatumia hayo mafuta yake, kwa sababu zeituni zitapukutika. 41Utakuwa na wana na binti lakini hawatakuwa nawe, kwa sababu watachukuliwa mateka.
Copyright information for
SwhKC